Monday, August 10, 2015

BAYERN INAPSWA KUIMARIKA ZAIDI - LAHM.

NAHODHA wa Bayern Munich Philipp Lahm amesisitiza kuwa kikosi chao kinapaswa kuimarika zaidi pamoja na ushindi mzuri wa mabao 3-1 waliopata dhidi ya Nottingen katika mchezo wa Kombe la Ujerumani jana. Mabao yaliyofungwa na Arturo Vidal, Mario Gotze na Robert Lewandowaski yalitosha kuwapa mabingwa ushindi dhidi ya timu hiyo ya daraja la chini. Hata hivyo, Lahm amesema bado wana safari ndefu ya kuimarika kwani hawakucheza kwa kiwango chao bora katika mchezo huo. Nahodha huyo aliongeza kuwa jambo la muhimu wamesonga mbele katika hatua inayofuata na hakuna mchezaji yeyote aliyeumia lakini ni wazi watalazimika kucheza vyema zaidi katika michezo mingine. Bayern watafungua pazia la Bundesliga kwa kucheza dhidi ya Hamburg Ijumaa hii.

No comments:

Post a Comment