Monday, August 10, 2015

CHELSEA HAIJUTII KUMKOSA PETR CECH - MOURINHO.

MENEJA wa Chelsea, Jose Mourinho amesema timu hiyo haijutii kumkosa golikipa Petr Cech na ana uhakika kikosi chake kitaendelea vyema pamoja na kumkosa Thibaut Courtois anayetumikia adhabu wakati watakapokuwa wageni wa Manchester City Jumapili ijao. Mourinho hakufurahishwa sana Cech mwenye umri wa miaka 33 kujiunga na mahasimu wao Arsenal baada ya kuwatumikia mabingwa hao kwa misimu 11 yenye mafanikio lakini meneja huyo amesisitiza ana furahia aina ya makipa aliobakiwa nao katika kikosi chake. Akihojiwa Mourinho amesema ana magolikipa wawili wazuri hivyo haoni kama kuna tatizo lolote kumkosa Cech. Cech aliamua kuhamia Arsenal baada ya kujikuta akikosa namba katika kikosi cha kwanza na kuchukuliwa na Courtois ambaye aliitwa na Chelsea kutoka Atletico Madrid alikokuwa kwa mkopo.

No comments:

Post a Comment