Monday, August 10, 2015

WENGER ADAI HATAKURUPUKA KUSAJILI.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amedai kuwa hatakurupuka kukimbilia sokoni kutafuta wachezaji wapya kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili wa kiangazi baada ya kipigo cha kushtusha kutoka kwa West Ham United jana. Golikipa Petr Cech ndio sura mpya pekee iliyotua Emirates katika kipindi hiki cha usajili na ameonekana kuanza vibaya kibarua chake hicho toka atoke Chelsea. Kuna tetesi kuwa Wenger ameshatenga fungu kwa ajili ya kumuwania mshambuliaji wa Real Madrid, Karim Benzema. Lakini meneja huyo amesema hatakurupuka kusajili kwasababu ya kupoteza mchezo wao kwanza katika ligi kwani jambo la msingi ni kuangalia walipokosea na kurekebisha.

No comments:

Post a Comment