Monday, August 10, 2015

NITAITENDEA HAKI JEZI NAMBA SABA - DEPAY,

MSHAMBULIAJI mpya wa Manchester United, Memphis Depay ana uhakika kuwa ataweza kuitendea haki jezi namba namba aliyopewa na klabu hiyo kama nyota wengine waliowahi kuivaa. Depay alipewa namba hiyo mashuhuri baada ya Angel Di Maria kuondoka kwenda Paris saint-Germain na kufuatia nyayo za nyota wengine waliowahi kuvaa jezi kama Cristiano Ronaldo, David Beckham, Eric Cantona na George Best. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa amesema yuko tayari kuitendea haki jezi hiyo kama ilivyokuwa kwa nyota wengine na kutamba kuwa atafanikiwa akiwa Old Trafford. Depay aliendelea kudai kuwa anafahamu changamoto yake na historia lakini ana uhakika ataendelea kuimarika zaidi na kupata mafanikio kama ilivyokuwa kwa wengine.

No comments:

Post a Comment