Tuesday, August 25, 2015

BEKI WA ZAMANI LA MADRID AMKINGIA KIFUA BENITEZ.

KIUNGO wa zamani wa Real Madrid, Ruben de la Red anaamini ni mapema mno kuhoji uwezo wa Rafael Benitez wa kuwa meneja wa klabu hiyo. Kufuatia matokeo mchanganyiko wakati wa maandalizi, Madrid wameanza rasmi mechi zake za mashindano chini ya Benitez aliyechukua nafasi ya Carlo Ancelotti kwa sare ya bila kufungana na Sportinh Gijon mwishoni mwa wiki iliyopita. Hata hivyo, De La Red amesema mashabiki wa Madrid wanapaswa kuwa wavumilivu na kocha huyo wa zamani wa Liverpool wakati huu akiwaongoza kwenda kunyakuwa taji lao kwanza la La Liga toka mwak 2012. De La Red aliendelea kudai kuwa Benitez anapaswa kupewa muda kwani kocha yeyote mpya hupitia katika kipindi hiki cha mpito katika kuwaelewesha wachezaji wake waweze kuzoea mbinu zake.

No comments:

Post a Comment