Tuesday, August 25, 2015

CITY WAPIGWA CHANGA LA MACHO KWA DE BRUYNE.

KIUNGO Kevin De Bruyne amefanya mazoezi na klabu yake ya Wolfsburg mchana wa leo pamoja na taarifa kuwa alitakiwa kusafiri kwenda nchini Uingereza kwa ajili ya kukamilisha uhamisho wake wenda Manchester City. Nyota huyo wa kimataifa wa Ubelgiji ni mmoja kati ya wachezaji City inaowaania na wiki iliyopita kuna taarifa zilizagaa zikidai kuwa City walikuwa tayari kuvunja rekodi ya usajili ili kumnasa kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili. Taarifa zilizozagaa nchini Uingereza leo ni kuwa De Bruyne alitarajiwa kusafiri kwenda jijini Manchester kumalizia uhamisho wake lakini kocha wa Wolfsburg Dieter Hecking alithibitisha kuwa nyota huyo atakuwepo mazoezini leo mchana. De Bruyne alijiunga na Wolfsburg Januari mwaka 2014 baada ya kushindw akung’aa katika klabu ya Chelsea chini ya Jose Mourinho.

No comments:

Post a Comment