Tuesday, August 25, 2015

HAMBURG WAMLILIA DJOUROU.

NAHODHA wa Hamburg SV Johan Djourou anatarajiwa kukosekana uwanjani kwa muda usijulikana baada ya kupata majeruhi ya paja katika mchezo wa Bundesliga dhidi ya VfB Stuttgart ambao walishinda mabao 3-2 Jumamosi iliyopita. Beki huyo wa kimataifa wa Uswisi mwenye umri wa miaka 28, alifunga bao katika dakika ya 89 ya kuisaidia timu yake kuibuka na ushindi huo wa kwanza dhidi ya Stuttgart. Klabu hiyo ilithibitisha kuumia kwa Djourou na kudai kuwa ni pigo kubwa kumkosa nahodha wao huyo tegemeo. Hamburg ambao wamelazimika kucheza hatua ya matoano kwa miaka miwili ili wabaki Bundesliga, Jumamosi hii wanapambana na Cologne.

No comments:

Post a Comment