Thursday, August 20, 2015

BAADA YA KUPIGWA BAO KWA PEDRO MAN UNITED SASA WAMGEUKIA MSENEGAL.

KLABU ya Southampton imekiri kuwa Manchester United wanamuwania winga wao wa kimataifa wa Senegal Sadio Mane. Wiki iliyopita Southampton walikanusha taarifa za kupokea ofa yeyote kwa ajili ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 23. Mshambuliaji wa Barcelona Pedro amekuwa akihisiwa kujiunga na United lakini kwa sasa yupo katika hatua za mwisho za kijiunga na Chelsea kwa dau la pauni milioni 21. Hivyo kufuatia hilo United wameamua kuongeza nguvu zao katika kumsajili mane kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili wa kiangazi. Mane amefunga mabao 10 katika mechi 32 alizocheza msimu uliopita baada ya kujiunga na klabu yake ya sasa akitokea Red Bull Salzburg ya Austria na yumo pia katika orodha ya wachezaji waliowahi kufunga magoli matatu -hat-trick kwa muda mfupi zaidi.


No comments:

Post a Comment