Thursday, August 20, 2015

PEDRO ATUA RASMI CHELSEA.

KLABU ya Chelsea imemsajili rasmi mshambuliaji wa Barcelona Pedro kwa kitita cha paundi milioni 21. Nyota huyo wa kimataifa wa Hispania katika siku za karibuni alionekana kama ataenda Manchester United lakini kushindwa kwao kufikia dau la euro milioni 30 lililotakiwa na Barcelona kumefanya mshambuliaji huyo kupata chaguo lingine. Mapema asubuhi Barcelona walithibitisha kuwa Pedro alikosa mazoezi ya klabu hiyo kwasababu ya kupewa ruhusa ya kwenda kukamilisha taratibu za uhamisho wake. Pedro ameitumikia Barcelona mechi 300 toka alipoibuka katika kikosi cha kwanza msimu wa 2007-2008, lakini ujio wa nyota wengine kama Neymar na Luis Suarez umemfanya mshambuliaji huyo kukosa nafasi ya kudumu katika kikosi cha kwanza. Pedro amekuwa mchezaji wa nne kusajiliwa na Chelsea baada ya Asmir Begovic, Radamel Falcao na Baba Rahman.

No comments:

Post a Comment