Wednesday, August 26, 2015

HISPANIA YAWA NCHI YA KWANZA KUINGIZA TIMU TANO CHAMPIONS LEAGUE.

HISPANIA imekuwa nchi ya kwanza kupata timu tano zilizofuzu hatua ya makundi ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kufuatia Valencia kufanikiwa kuichapa Monaco katika mechi ya mtoano. Valencia waliowahi kuwa washindi wa pili wa michuano hiyo mwaka 2001, ambao wana beki wa zamani wa Manchester United katika benchi lao ufundi, wanaungana na Real Madrid, Barcelona na Atletico Madrid. Sevilla wao pia watakuwepo katika ratiba hiyo ya makundi wakifuzu kama mabingwa wa michuano ya Europa League msimu uliopita. Ratiba ya makundi ya michuano hiyo inatarajiwa kupangwa rasmi kesho. Huu ni msimu wa kwanza kuwepo uwezekano wan chi moja kuwa na timu tano kati ya timu 32 zitakazokuwepo katika hatua ya makundi toka Shirikisho la Soka la Ulaya-UEFA kutangaza kuwa mshindi wa Europa League pia atapata nafasi ya moja kwa moja kucheza Ligi ya Mabingwa msimu unaofuata.

No comments:

Post a Comment