Wednesday, August 26, 2015

MASCHERANO AUTAKA UKOCHA AKISTAFU.

KIUNGO wa Barcelona, Javier Mascherano amebainisha kuwa anataka kuwa kocha wakati atapoamua kutundika daruga zake. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 31 ana miaka mitano Barcelona toka ahamie akitokea Liverpool mwaka 2010 baada pia ya kuzitumikia West Ham United, Corinthians na River Plate. Akihojiwa Mascherano ambaye kwasasa ni nahodha msaidizi wa Barcelona amesema anataka kuwa kocha pindi atakapostaafu soka ingawa anafahamu haitakuwa kazi rahisi. Nyota aliendelea kudai kuwa ukiwa mchezaji mambo huwa sio magumu sana lakini huwa yanabadilika unapohamia upande wa pili lakini anafahamu anaweza kukabiliana na changamoto zozote kutokana na uzoefu wake.

No comments:

Post a Comment