Wednesday, August 26, 2015

VIDAL ADAI WACHEZAJI SASA WANALIPWA SANA KULIKO VIWANGO VYAO.

KIUNGO wa Bayern Munich, Arturo Vidal amesema ada zinazolipwa na klabu kwa ajili ya kusajili wachezaji ni kubwa sana, na kudai kuwa baadhi yao wanapaswa kufunga walau mabao matatu au manne ili kufikia thamani hiyo. Vidal mwenyewe alitua Bayern akitokea Juventus kwa kitita kikubwa kilichofikia euro milioni 40 Julai mwaka huu. Akihojiwa Vidal amekiri kuwa wachezaji wachache sana ndio wanastahili kununuliwa kwa thamani hiyo katika soka hili la kisasa. Vidal aliendelea kudai kuwa kwa mtazamo wake gharama hizo zilipaswa kushuka ili kupunguza shinikizo kwa baadhi ya wachezaji.

No comments:

Post a Comment