Wednesday, August 26, 2015

VALENCIA AITUHUMU WEST HAM KUMTENGA.

MSHAMBULIAJI wa West Ham United, Enner Valencia amekasirishwa na klabu yake hiyo, akiamini kuwa imemtelekeza toka apate majeruhi. Nyota huyo wa kimataifa wa Ecuador aliumia mguu wakati wa mchezo wa Europa League dhidi ya Astra Giurgiu Agosti 2 mwaka huu na sasa anatakiwa kukaa nje ya uwanja kwa miezi mitatu. Hata hivyo, Valencia ambaye alifunga mabao manne katika Ligi Kuu msimu uliopita, amedai amekuwa akiwekwa gizani kuhusu maendeleo yake na kuituhumu klabu hiyo kumzuia kwenda kujitafutia matibabu yake mwenyewe. Akihojiwa Valencia amesema West Ham wanaonekana wamemsahau kama ameumia kwani hawataki kumruhusu kuzungumza na madaktari wengine na hajui kwanini madaktari wa timu hiyo wanamfanyia hivyo.

No comments:

Post a Comment