Wednesday, August 26, 2015

BALOTELLI APIGWA MKWARA MZITO AC MILAN.

MSHAMBULIAJI mahiri wa kimataifa wa Italia, Mario Balotelli amewekewa sheria kali katika mkataba wake wa mkopo na klabu ya AC Milan, akizuiwa kunyoa na kuvaa nguo za kiajabuajabu na pia akitakiwa kuishi maisha bora. Vyombo vya habari nchini Italia vimedai kuwa Ofisa Mkuu wa klabu hiyo Andriano Galliani amemuwekea sheria hizo ambazo mara nyingi hutumika kwa watu wanatumikia jeshi la nchi hiyo. Balotelli mwenye umri wa miaka 25 ambaye mara kadhaa amekuwa akikosolewa kwa kushindwa kujituma anatarajiwa kuanza kuitumikia Milan tena ikiwa ni mwaka mmoja toka aondoke kwenda Liverpool ambako nako alishindw akung’aa. Inadaiwa kuwa mbali na kuzuiwa kuvaa na kunyoa kiajabuajabu Balotelli pia hatatakiwa kuvuta sigara, kufanya starehe katika vilabu vya usiku kupiliza pamoja na unywaji pombe.

No comments:

Post a Comment