Wednesday, August 26, 2015

ARSENAL WAPANGIWA MAHASIMU WAO TOTTENHAM HOTSPURS KOMBE LA LIGI.

KLABU ya Tottenham Hotspurs itakuwa wenyeji wa mahasimu wao wa kaskazini ya London Arsenal katika mchezo wa mzunguko wa tatu wa Kombe la Ligi. Mabingwa Chelsea wao wataanza kutetea taji lao kwa kusafiri kuifuata Walsall inayoshiriki ligi daraja la kwanza wakati Aston Villa wao wamepangwa na mahasimu wao Birmingham City. Katika mechi zingine, Manchester United na Liverpool zimepewa mechi za nyumbani dhidi ya Ipswich Town na Carlisle. Hatua hiyo itakuwa na mechi zingine tatu zitakazohusisha timu za Ligi kuu ambapo Sunderland wao watakuwa wenyeji wa Manchester City, Norwich watachuana na West Bromwich Albion na Leicester City wakiivaa West Ham United.

No comments:

Post a Comment