Thursday, August 27, 2015

OZIL ATAKA SCHWEINSTEIGER APEWE MUDA ILI KUONYESHA MAKALI YAKE.

KIUNGO wa Arsenal, Mesut Ozil anaamini Mjerumani mwenzake Bastian Schweinsteiger anakosolewa visivyo kufuatia uhamisho wake kwenda Manchester United. Kumekuwa na mijadala ya aidha mwili wa Schweinsteiger mwenye umri wa miaka 31 kama utaweza kukabiliana na mikikimikiki ya Ligi Kuu baada ya kuondoka Bayern Munich Julai mwaka huu. Mpaka sasa kiungo huyo hajapata nafasi ya kucheza dakika zote tisini kwani amekuwa aidha akianza na kutolewa katikati au kuingia baada ya muda wa mapumziko katika mechi kadhaa za United zilizopita. Akihojiwa Ozil amesema hana shaka kabisa kuwa Schweinsteiger atawanyamazisha wale wote wanaomkosoa kwa kuonyesha kiwango bora pindi wakati utakapowadia. Ozil aliendelea kudai kuwa kwasasa ni mapema mno kukosoa kiwango chake kwani anamfahamu vyema uwezo wake.

No comments:

Post a Comment