Thursday, August 27, 2015

BALOTELLI AKIRI KUACHA MAMBO YA KITOTO.

MSHAMBULIAJI nyota Mario Balotelli amesema hawezi kufanya makosa zaidi hivi sasa baada ya kurejea AC Milan kwa mkopo. Nyota huyo wa kimataifa wa Italia, mwenye umri wa miaka 25 amereje Milan akitokea Liverpool alipocheza kwa msimu mmoja pekee. Akihojiwa Balotelli amekiri kupoteza nafasi nyingi alizopata kutokana na mambo yasiyokuwa na umuhimu jambo ambalo limemrudisha nyuma kwa kiasi fulani. Nyota huyo amesema hajasahau kucheza soka na kwasasa amepevuka na sio mtoto tena hivyo ana uhakika wa kurejea katika ubora wake. Balotelli alifanikiwa kufunga bao moja pekee katika Ligi Kuu akiwa Liverpool baada ya kusajiliwa kwa kitita cha paundi milioni 16 kutoka Milan Agosti mwaka 2014.

No comments:

Post a Comment