Thursday, August 27, 2015

ROONEY AANZA KUCHONGA BAADA YA KUPIGA HAT-TRICK.

NAHODHA wa Manchester United, Wayne Rooney amesema ana uzoefu wa kutosha wa kukabiliana na wanaomkosoa baada ya kumaliza ukame wa kutofunga bao katika mechi 10 alizoichezea timu hiyo. Mshambuliaji huyo anaonekana kurejesha makali yake baada ya kuanza msimu kwa kusuasua, akifunga mabao matatu hat-trick katika ushindi wa mabao 4-0 waliopata United dhidi ya Club Brugge katika mechi ya kufuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo uliochezwa jana usiku, Rooney amesema kama asingekuwa imara jambo hilo lingeweza kumuathiri lakini anafahamu uwezo wake. Ushindi unaifanya United kujihakikishia nafasi ya kuwepo katika ratiba ya makundi ya michuano hiyo baada ya kukosa kushiriki msimu uliopita.

No comments:

Post a Comment