Thursday, August 27, 2015

WENGER AKIRI USAJILI UNAMNYIMA USINGIZI.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amethibitisha kuwa wanafanya kazi saa 24 kuangalia uwezekano wa kufanya usajili kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili la kipindi hiki cha kiangazi. Klabu hiyo imefanikiwa kumsajili Petr Cech pekee kutoka Chelsea kipindi hiki huku wachezaji wengine waliokuwa wakiwaania Karim Benzema na Grzegorz Krychowiak wakithibitisha kubakia katika vilabu vya Real Madrid na Sevilla. Pamoja na kushindwa kuongeza wachezaji katika nafasi ya kiungo na ushambuliaji, Wenger amedokeza kuwa timu yake ya usajili inahaha kutafuta wachezaji mahali popote watakaofaa. Wenger amesema wamekuwa wkifanya kazi saa 24 kuhakikisha wanapata wachezaji sahihi watakaofaa ili kuimarisha kikosi chake kwa ajili ya msimu huu.

No comments:

Post a Comment