Thursday, August 27, 2015

SPURS YAMUWANIA NYOTA WA KOREA KUSINI.

KLABU ya Tottenham Hotspurs iko katika mazungumzo ya kuwania kumsajili mshambuliaji wa Bayer Leverkusen Son Heung-min. Nyota huyo wa kimataifa wa Korea Kusini mwenye umri wa miaka 23, amefunga mabao 21 kati ya mechi 62 za Bundesliga alizocheza toka ajiunge na Leverkusen akitokea Hamburg mwaka 2013. Inaaminika kuwa Spurs wamepanga kutoa kitita cha paundi milioni 22 kwa ajili ya kunasa saini ya Son. Spurs wanafanya hivyo kufuatia ofa yao ya pili kwa mshambuliaji wa West Bromwich Albion Saido Berahino kukataliwa.

No comments:

Post a Comment