Thursday, August 27, 2015

BAYERN YAMUONGEZA MKATABA THIAGO.

KLABU ya Bayern Munich imethibitisha kiungo wao Thiago Alcantara ameongeza mkataba mwingine mpya ambao utamalizika mwaka 2019. Kiungo huyo alijiunga na Bayern akitokea Barcelona mwaka 2013 ambapo aliungana na kocha Pep Guardiola waliyekuwa naye Camp Nou. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 amekuwa akisumbuliwa na majeruhi kwa kipindi kirefu alichokuwa Ujerumani lakini alionyesha kiwango bora pindi alipokuwa fiti jambo ambalo limemfanya kupewa mkataba mwingine. Ofisa mkuu wa Bayern, Karl-Heinz Rummenigge amesema amefurahishwa na taarifa hizo kwani Thiago bado ni mchezaji mdogo hivyo atakuwa hazina nzuri kwa timu hiyo ziku za baadae. Thiago amecheza mechi 25 pekee za Bundesliga toka atue Bayern huku akifunga mabao mawili.

No comments:

Post a Comment