Thursday, August 27, 2015

BOLT ADHIHIRISHA UFALME WAKE BEIJING.

MWANARIADHA nyota wa mbio fupi wa Jamaica, Usain Bolt amefanikiwa tena kutetea ubingwa wake dunia kwa kunyakuwa medali ya dhahabu katika mbio za 200 zilizofanyika leo. Bolt ambaye pia alifanikiwa kutetea ubingwa wake katika mbio za mita 100 Jumapili iliyopita alifanikiwa kushinda mbio hizo za leo akitumia muda wa sekunde 19.55 ukiwa ni muda bora mwaka huu. Mpinzani wake wa karibu ambaye alikuwa akipewa nafasi kubwa ya kushinda Bolt, Justin Gatlin wa Marekani alishika nafasi ya pili na kupata medali ya fedha akitumia muda wa sekunde 19.74. Nyota kutoka Afrika Kusini Anaso Jobodwana alishika nafasi ya tatu katika mbio hizo.

No comments:

Post a Comment