Friday, August 28, 2015

SON AMWAGA WINO SPURS.

KLABU ya Tottenham Hotspurs imefanikiwa kukamilisha usajili wa mshambuliaji Son Heung-min kutoka klabu ya Bayer Leverkusen ya Ujerumani. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 ana rekodi ya kufunga mabao 29 katika mechi 87 alizoichezea Leverkusen toka ajiunge akitokea Hamburg mwaka 2013. Spurs inaripotiwa kutoa kitita cha paundi milioni 22 kwa ajili ya kunasa saini ya nyota huyo huku wakimpa mkataba wa mpaka mwaka 2020. Klabu hiyo pia imeshuhudia ofa zake mbili kwa ajili ya kumuwania Saido Berahino zikitupiliwa mbali na West Bromwich Albion ambao wamedai hawana mpango wa kumuuza nyota huyo mwenye umri wa miaka 22. Kukataliwa huko kumsajili Berahino ndio kunatajwa kuchangia kwa kiasi kikubwa Spurs kumgeukia Son.

No comments:

Post a Comment