Wednesday, August 19, 2015

PIQUE ALIMWA ADHABU YA MECHI NNE PAMOJA NA KUOMBA RADHI.

BEKI wa Barcelona, Gerard Pique ameomba radhi kufuatia kutolewa kwake katika mchezo wa maruadiano wa Super Cup dhidi ya Athletic Bilbao lakini amekanusha kumtukana mwamuzi msaidizi. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 28, alimavaa mwamuzi msaidizi na kumzonga wakati wa mchezo wao dhidi Bilbao ambao ulimalizika kwa sare ya bao 1-1 katika Uwanja wa Camp Nou. Pique aliandika katika ukurasa wake wa mtandao kijamii wa twitter akiomba radhi kwa tukio hilo lakini alikanusha kumtukana mwamuzi huyo kama ilivyofikiriowa na wengi. Hata hivyo pamoja na Pique kuomba radhi, Shirikisho la Soka la Hispania limemlima adhabu ya kutocheza mechi nne beki huyo leo. Barcelona wanatarajiwa kuanza kutupa karata yao ya kwanza ya kutetea taji lao la La Liga kwa kuvaana tena na Bilbao Jumapili hii.

No comments:

Post a Comment