Wednesday, August 19, 2015

LIVERPOOL ITALIPA KISASI DHIDI YA ARSENAL - LALLANA.

KIUNGO wa Liverpool, Adam Lallana amesema timu hiyo imesuka mipango kabambe ya kuibuka na ushindi ugenini wakati watakapokwenda kuchuana na Arsenal katika Uwanja wa Emirates Jumatatu ijayo. Liverpool wameshinda mechi zao zote mbili za Ligi Kuu msimu huu na Lallana amesema meneja wao Brendan Rodgers amepanga kupata alama zote tatu kutoka kwa mahasimu wao hao. Lallana mwenye umri wa miaka 27 aliendelea kudai kuwa Rodgers amewapanga kwenda kupata matokeo katika mchezo huo. Arsenal waliichapa Liverpool mabao 4-1 msimu uliopita lakini Lallana anaamini matokeo hayo hayataweza kujirudia tena safari hii.

No comments:

Post a Comment