Monday, August 17, 2015

BENITEZ AMTAKA BENZEMA KUFUNGA MABAO 25 MSIMU HUU.

MENEJA wa Real Madrid, Rafa Benitez anataka mshambuliaji wake Karim Benzema kufunga walau mabao 20 msimu huu. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa, amekuwa akihusishwa na tetesi za kwenda Arsenal katika wiki za karibuni huku meneja wa timu hiyo Arsenal Wenger akiwa na matumaini ya kumsajili kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili wa kiangazi mwishoni mwa mwezi huu. Benzema amefunga mabao 22 katika mashindano yote msimu uliopita lakini benitez anadhani nyota huyo mwenye umri wa miaka 27 anaweza kufanya zaidi katika msimu huu wa 2015-2016. Akihojiwa Benitez amesema Benzema ni mchezaji mkubwa na moja ya malengo aliyonayo juu yake ni kumtaka ajitahidi kufunga mabao zaidi kati ya 20 mpaka 25 ana uhakika hilo liko ndani uwezo wake.

No comments:

Post a Comment