Monday, August 17, 2015

CHUNG MONG-JOON ATANGAZA RASMI KUGOMBEA URAIS FIFA.

MFANYABIASHARA na mwanasiasa maarufu nchini Korea Kusini Chung Mong-joon ametangaza rasmi nia yake ya kugombea nafasi ya urais wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA katika uchaguzi utakaofanyika mwakani. Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Februari 26 baada ya rais wa sasa Sepp Blatter kutangaza nia yake ya kuachia ngazi Juni mwaka huu kufuatia kashfa ya ufisadi iliyolikumba shirikisho hilo. Blatter alichaguliwa tena kuongoza muhula wa tano wakati kashfa hiyo ilipoibuka lakini baadae alithibitisha rasi mpya atachaguliwa katika mkutano mkuu usio wa kawaida utakaofanyika Februari. Akizungumza na wana habari jijini Paris kutangaza nia yake hiyo, Chung ambaye pia ni makamu wa rais wa heshima wa FIFA, amesema FIFA inahitaji kiongozi ambaye ataleta uaminifu, uwazi na uwajibikaji. Chung mwenye umri wa miaka 61 aliendelea kudai kuwa ili shirikisho lifanikiwa kupiga teke ufisadi ni lazima liweze kupata mabadiliko ya mara kwa mara katika uongozi. Mbali na Chung, wengine waliotangaza nia ya kugombea nafasi hiyo mpaka sasa ni pamoja na rais wa Shirikisho la Soka la Ulaya-UEFA Michel Platini, nguli wa soka wa zamani wa Brazil, Zico na rais wa Shirikisho la Soka la Liberia Musa Bility.

No comments:

Post a Comment