Monday, August 17, 2015

PELLEGRINI AANZA KUCHONGA, ADAI WACHEZAJI WAKE WANA HASIRA NA NJAA YA USHINDI.

MENEJA wa Manchester City, Manuel Pellegrini amesema wachezaji wake wana njaa na kiu baada ya kulikosa taji la Ligi Kuu msimu uliopita. City walimaliza katika nafasi ya pili msimu uliopita nyuma ya mabingwa Chelsea wakitofautiana kwa alama nane. Akihojiwa mara baada ya kikosi chake kuichapa Chelsea kwa mabao 3-0 jana, Pellegrini amesema pengine kilichotokea msimu uliopita kilikuwa ni uzoefu tosha kwao. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa wachezaji wake hivi sasa wana njaa na kiu ndio maana wanataka kushinda katika kila mchezo. Mabao ya City katika mchezo huo yalifungwa na Sergio Aguero, nahodha Vincent Kompany na Fernandinho.

No comments:

Post a Comment