Monday, August 17, 2015

MOURINHO ATETEA UAMUZI WAKE WA KUMTOA TERRY.

MENEJA wa Chelsea, Jose Mourinho ametetea uamuzi wake wa kumuondoa nahodha John Terry wakati wa mapumziko kufuatia kipigo cha mabao 3-0 walichopata kutoka kwa Manchester City jana. Beki huyo mkongwe mwenye umri wa miaka 34 alibadilishwa na nafasi yake kuchukuliwa na Kurt Zouma huku City wakiwa tayari wanaongoza kwa bao 1-0 katika kipindi cha kwanza. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo, Mourinho alithibitisha kuwa Terry hakuumia katika mchezo huo na kumtoa kwake ilikuwa sehemu ya mipango yake. Mourinho amesema ilikuwa wazi kwake kuwa Zouma alitakiwa kucheza katika mechi hiyo. Terry ameshinda mataji manne ya Ligi Kuu, matano ya Kombe la FA, moja la Ligi ya Mabingwa Ulaya na moja la Europa League katika kipindi cha miaka 17 ambayo ameitumikia Chelsea.

No comments:

Post a Comment