Monday, August 17, 2015

RAMOS AKUBALI KUSAINI MKATABA MPYA.

HATIMAYE beki mahiri Sergio Ramos aliyekuwa akiwaniwa na klabu ya Manchester United, amekubalia kusaini mkataba mpya wa miaka mitano na timu yake ya Real Madrid. United walituma ofa ya paundi milioni 28.6 kwa ajili ya beki huyo mwenye umri wa miaka 29 mapema kiangazi hiki wakati mazungumzo ya mkataba wake yalipokuwa yakisuasua. Hata hivyo, nyota huyo wa kimataifa wa Hispania sasa atabakia Madrid baada ya kuonekana akiwa sambamba na rais Florentino Perez katika shughuli za kusaini mkataba huo. Mkataba mpya wa Ramos utamfanya kuendelea kuwepo Santiago Bernabeu mpaka mwaka 2020. Akihojiwa mara baada ya kusaini mkataba huo Ramos amesema fedha sio sababu iliyomfanya kuongeza mkataba mwingine katika timu hiyo. Nyota huyo aliendelea kudai kuwa angeweza kupata fedha nyingi zaidi kama angeamua kuondoka kwenda kwingine lakini kunatokana na mapenzi aliyonayo kwa Madrid asingeweza kufanya hivyo.

No comments:

Post a Comment