Friday, August 28, 2015

SCHMEICHEL AMSIHI DE GEA ABAKI UNITED.

GOLIKIPA wa zamani wa Manchester United, Peter Schmeichel amemtaka David de Gea kusaini mkataba na klabu hiyo, kutokana na uwezekano wake kuhamian Real Madrid kuwa mdogo. Suala la De Gea linatarajiwa kwenda mpaka siku ya mwisho ya usajili wa kiangazi kutokana na United na Madrid kuonekana kuendelea kuvutana kufikia muafaka wa usajili wa kipa huyo ambye mpaka sasa hajajumuishwa katika kikosi cha Louis van Gaal msimu huu. Van Gaal amesisitiza De Gea hatauzwa mpaka dirisha la usajili litakapofungwa pamoja na mkataba wa nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 kukaribia kumalizika mwishoni mwa msimu huu. Schmeichel anaonekana kuchoshwa na suala hilo na anataka De Gea kuendelea kuitumikia United msimu huu. Schmeichel aliendelea kudai kuwa De Gea amekuwa katika kiwango kizuri katika msimu miwili iliyopita hivyo angefurahi kama angesaini mkataba mwingine wa miaka mitano Old Trafford.

No comments:

Post a Comment