Thursday, September 24, 2015

MZUNGUKO WA NNE CARLING CUP: ARSENAL KUIVAA SHEFFIELD, CITY VS PALACE, CHELSEA VS STOKE.

KLABU ya Arsenal intarajiwa kuwa mgeni wa timu ya daraja la pili ya Sheffield Wednesday katika mchezo wa mzunguko wa nne wa michuano ya Kombe la Ligi. Wednesday walipata bahati ya kusonga mbele kufuatia kuichapa Newcastle United bao 1-0 katika Uwanja wa St James Park huku Arsenal wao wakiwaondosha majirani zao Tottenham Hotspurs kwa kuwafunga mabao 2-1. Baada ya kupenya kwa matuta dhidi ya timu ya daraja la nne ya Carlisle, Liverpool wao sasa watakutana na Bournemouth ambao wamepanda Ligi Kuu msimu huu. Kwa upande mwingine vinara wa Ligi Kuu Manchester City wao wataivaa Crystal Palace, wakati mabingwa watetezi wa michuano hiyo Chelsea wao watakuwa wageni wa Stoke City. Manchester United wao watakuwa wenyeji wa Middlesbrough baada ya kuichapa Ipwich Town kwa mabao 3-0.

No comments:

Post a Comment