Thursday, September 24, 2015

BAYERN YAMTENGEA FUNGU NENE GUARDIOLA.

OFISA mkuu wa Bayern Munich, Karl-Heinz Rummenigge amebainisha klabu hiyo imemtengea ofa nono Pep Guardiola na wana uhakika kocha huyo atasaini mkataba mpya na mabingwa hao wa Bundesliga. Mkataba wa sasa wa Guardiola unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu na mpaka sasa hakuna mazungumzo yeyote yalioanza jambo ambalo linazua tetesi za uwezekano wa kocha huyo kuondoka. Pamoja na hayo, Rummenigge anaamini meneja huyo wa zamani wa Barcelona atapata wakati mgumu ofa nono waliyomtengea. Rummenigge amesema ana uhakika Guardiola ataongeza mkataba mwingine kwani fungu walilomtengea ni kubwa na hadhani kama anaweza kulikataa.

No comments:

Post a Comment