Thursday, September 24, 2015

BARUA PEPE ZA VALCKE KUPEKULIWA.

WACHUNGUZI wa Switzerland wamelitaka Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kuwapa kibali cha kupekua barua pepe za katibu mkuu wa shirikisho hilo aliyesimamishwa Jerome Valcke. Baadhi ya magazeti yamekuwa yakimtuhumu Valcke mwenye umri wa miaka 54, kuuza tiketi za Kombe la Dunia kwa bei ya juu tofauti iliyopangwa. Toka wakati huo Valcke amesimamishwa kibarua chake hicho akipisha uchunguzi. Katika taarifa ya kamati inayoongoza uchunguzi huo imedai kuwa wanataka kibali toka FIFA kwani kwasasa barua pepe hizo zitakuwa chini yao. Valcke raia wa Ufaransa ambaye ameshikilia wadhifa huo toka mwaka 2007 amekanusha madai hayo.

No comments:

Post a Comment