Thursday, September 24, 2015

TOURE AWASIF KINA DE BRUYNE NA STERLING.

KIUNGO Yaya Toure anaamini Manchester City sasa wana kikosi kinachovutia zaidi Ulaya kufuatia usajili wa majira ya kiangazi wa Kevin De Bruyne na Raheem Sterling. City wanaongoza Ligi Kuu kwa tofauti ya alama mbili baada ya kucheza michezo sita huku wakitumia karibu paundi milioni 100 kununua wachezaji wapya. Wawili kati ya wachezaji walionunuliwa tayari wameshaanza kuonyesha makali yao na Toure amewamwagia sifa kwa kuipa timu hiyo chaguo zaidi katika safu ya ushambuliaji. Toure amesema De Bruyne ni mchezaji mwenye kipaji cha kipekee kwani ana uwezo wa kutengeneza nafasi za mabao huku na yeye mwenyewe akifunga kama alivyofanya katika mchezo wao dhidi ya Sunderland. Kiungo huyo aliendelea kudai kuwa pia yupo Sterling na Sergio Aguero kitendo ambacho kinafanya safu yao ya ushambuliaji kuwa hatari zaidi kwasasa.

No comments:

Post a Comment