Thursday, September 24, 2015

MOURINHO AIKOSOA FA.

MENEJA wa Chelsea, Jose Mourinho amekikosoa Chama cha Soka cha Uingereza-FA kufuta kadi nyekundu aliyopewa beki wa Arsenal Gabriel. Beki huyo alilimwa kadi nyekundu kwa kosa la kumkwatua Diego Costa kwa nyuma katika ushindi wa mabao 2-0 iliyopata Chelsea dhidi ya Arsenal. Akihojiwa kuhusiana na hilo Mourinho amesema sasa wanafahamu kuwa kitendo cha kulipiza kisasi kinaruhusiwa kutokana na hatua zilizochukuliwa na FA. Kocha huyo pia aligoma kuzungumzia adhabu ya mechi tatu aliyopewa Costa akidai kuwa kama akifanya hivyo adhabu kubwa dhidi yake ingekuwa ikimsubiri. Kwa upande wake meneja wa Arsenal Arsene Wenger amesema FA wametatua tatizo hilo kwa asilimia tano.

No comments:

Post a Comment