Friday, September 25, 2015

NEYMAR AKIRI KUFANYA MAZUNGUMZO NA UNITED.

MSHAMBULIAJI wa Barcelona, Neymar amethibitisha kufanya mazungumzo na Manchester United lakini hakuna ofa yeyote iliyotolewa. Nyota huyo wa kimataifa wa Brazil, ambaye alikuwa sehemu ya kikosi cha Barcelona akifunga mabao 22 msimu uliopita na kupelekea kunyakuwa mataji matatu alikuwa akihuishwa na tetesi za kwenda United waliokuwa wakihitaji mshambuliaji kabla ya kumsajili Anthony Martial. Akihojiwa kuhusiana na hilo na ESPN Neymar amesema ni kweli kulikuwa na mazungumzo lakini hakuna ofa yeyote iliyowekwa mezani na United. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 aliongeza kuwa lengo lake kubwa ni kubakia Barcelona na kushirikiana na wenzake kunyakuwa mataji mengi kadri wawezavyo. Barcelona ambao wataikaribisha La Palmas kesho katika mchezo wa La Liga wanashika nafasi ya tano katika msimamo kufuatia kipigo cha mabao 4-1 walichopata kutoka kwa Celta Vigo.

No comments:

Post a Comment