Sunday, September 27, 2015

RONALDO ASHINDWA KUIBEBA MADRID.

MSHAMBULIAJI nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo jana alishindwa kuifungia timu yake bao na kujikuta wakitoa sare ya bila kufungana dhidi ya Malaga na kupoteza nafasi yao ya kuongoza La Liga. Nyota huyo wa kimataifa wa Ureno anahitaji mabao matatu pekee kuipita rekodi ya Raul ya mabao 323 na kuweka rekodi mpya ya ufunguzi. Lakini pamoja na Madrid kumiliki sehemu kubwa ya mchezo wa jana, Ronaldo alishindwa kabisa kutikisa nyavu huku akikosa bao la wazi katika dakika za majeruhi. Malaga ilibidi wafanye kazi ya ziada kujilinda katika dakika 13 za mwisho baada ya Nordin Amrabat kulimwa kadi nyekundu kwa kosa la kumpiga kiwiko beki wa Madrid Marcelo. Ronaldo mwenye umri wa miaka 30 ametumia mechi 306 alizocheza kufunga mabao 321 wakati Raul yeye alitumia mechi 741 alizocheza kuweka rekodi yake.

No comments:

Post a Comment