Sunday, September 27, 2015

NYOTA YA LEWANDOWSKI YAZIDI KUNG'AA BAYERN.

WIKI ya kukumbukwa kwa Robert Lewandowski imeendelea tena wakati mshambuliaji alipofikisha rekodi ya mabao 100 katika Bundesliga ambayo ni haraka zaidi kuliko mchezaji yeyote wa kigeni. Nyota huyo wa kimataifa wa Poland mwenye umri wa miaka 27, alifunga mabao matano ndani ya muda wa dakika tisa katika mchezo wa katikati ya wiki dhidi ya Wolfsburg na kufunga mabao mengine mawili zaidi dhidi ya Mainz na kuifanya Bayern kushinda mechi zao zote saba za ligi mpaka sasa. Lewandowski amefikia rekodi hiyo ya mabao 100 katika mechi 168 alizocheza rekodi ambayo haijafanywa na mchezaji yeyote wa kigeni katika Bundesliga. Sasa nyota hhuyo ambaye alisajiliwa Bayern kama mchezaji huru, amefikisha mabao 10 msimu huu na kumfanya kuwa mchezaji wa pili katika historia ya Bundesliga baada ya nguli wa zamani Gerd Muller kufikisha idadi hiyo katika mechi saba za mwanzo wa msimu.

No comments:

Post a Comment