Sunday, September 27, 2015

WENGER AMSIFU SANCHEZ BAADA YA HAT-TRICK.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema Alexis Sanchez amerejea katika ubora wake baada ya kufunga hat-trick katika mchezo wa Ligi Kuu walioibuka na ushindi wa mabao 5-2 dhidi ya Leicester City jana. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Chile amekua akisuasua msimu huu baada ya kufunga mabao 25 katika msimu wake kwanza akiwa na Arsenal baada ya kuondoka Barcelona. Wenger amesema alikuwa anafahamu kuwa itachukua muda kidogo kwa Sanchez kurejea katika ubora haswa kutokana na kupata mafanikio makubwa na timu yake ya taifa katika michuano ya Copa Amerika iliyomalizika mapema kiangazi. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa katika siku zijazo Sanchez ataweza kuwa hatari zaidi kwani amekuwa akijituma kwa bidii bila kuchoka.

No comments:

Post a Comment