Sunday, September 27, 2015

MOURINHO AKIPONDA KIKOSI CHAKE.

MENEJA wa Chelsea, Jose Mourinho amekipa kikosi chake hasi moja katika maksi kumi kutokana na kiwango kibovu walichoonyesha katika kipindi cha kwanza na kupelekea kuambulia sare ya mabao 2-2 dhidi ya Newcastle United jana. Mourinho alishuhudia kikosi chake kikiimarika kwa kutoka nyuma na kufanikiwa kupata walau alama moja lakini walionekana kucheza hovyo katika kipindi cha kwanza. Akihojiwa kocha huyo amesema walicheza vibaya sana katika kipindi cha kwanza hatua ambayo ilimfanya kutaka kufanya walau mabadiliko sita badala ya matatu kama sheria zinavyotaka. Hata hivyo, Mourinho anashukuru kipindi cha pili waliimarika na kucheza vyema huku akiwapongeza viungo wake Willian na Ramirez kwa kuonyesha kiwango cha juu. Mourinho amesema wachezaji hao waliongeza nguvu kwa kikosi chake kutokana na kasi yao jambo ambalo Newcastle walishindwa kulimudu.

No comments:

Post a Comment