Sunday, September 27, 2015

EVRA ADAI WANAPASWA KUJILAUMU WENYEWE KWA MATOKEO MABOVU.

BEKI wa Juventus, Patrice Evra amesema hawana la kujitetea kwa timu yao kuanza kwa kusuasua msimu huu baada ya kukubali kipigo kingine jana. Kikosi cha Juventus kilichochini ya Massimiliano Allegri kilifanyiwa mabadiliko kiangazi kufuatia kuondoka kwa Andrea Pirlo, Arturo Vidal na Carlos Tevez, wakati majeruhi pia yamekuwa yakiwasumbua mapema msimu huu ambapo Claudio Marchisio na kiungo mpya Sami Khedira wakitarajiwa kukaa nje ka kipindi kirefu. Mabingwa hao watetezi walijikuta wakitandikwa mabao 2-1 na Napoli jana na kuwaacha wakiwa wamepata ushindi mmoja katika mechi zao sita za mwanzo na kuwafanya kuwa nyuma ya vinara Inter Milan kwa tofauti ya alama 10. Akihojiwa Evra amesema wachezaji chipukizi wengi waliopo katika kikosi chao hawapaswi kuchukuliwa kama sababu ya wao kufanya vibaya kwani wao wazoefu ndio wenye wajibu wa kuwasaidia. Beki huyo aliendelea kudai kuwa ni wakatu mgumu kwao hivi sasa na inaumiza lakini hawatakiwa kuchanganyikiwa kwasasa kwani mambo yanaweza kwenda mrama zaidi.

No comments:

Post a Comment