Sunday, September 27, 2015

MAJERUHI KUMUWEKA MESSI NJE WIKI NANE.

MSHAMBULIAJI wa Barcelona, Lionel Messi anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa muda wa wiki saba mpaka nane baada ya kuumia goti lake la kushoto katika mchezo wa La Liga walioshinda mabao 2-1 dhidi ya Las Palmas jana. Messi mwenye umri wa miaka 28 aliumia dakika ya tatu ya mchezo na kukimbizwa moja kwa moja hospitali baada ya kubalidishwa. Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina anatarajiwa kukosa mechi nane zijazo za Barcelona lakini anaweza kurejea kwa wakati kwa ajili ya mchezo El Classico dhidi ya mahasimu wao Real Madrid Novemba 22 mwaka huu. Akihojiwa meneja wa Barcelona, Luis Enrique amesema siku zote amekuwa na majonzi pindi wachezaji wake wanapoumia na anahuzunikaga zaidi mchezaji huyo anapokuwa Messi.

No comments:

Post a Comment