Monday, September 28, 2015

AUBAMEYANG AWEKA HISTORIA BUNDESLIGA.

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Gabon, Pierre-Emerick Aubameyang amekuwa mchezaji wa kwanza kufunga mabao katika mechi zote saba za Bundesliga wakati Borussia Dortmund walipotoa sare dhidi ya Darmstadt. Katika mchezo huo Aubameyang alifunga mabao mawili katika dakika ya 63 na 71 katika sare ya mabao 2-2 waliyopata katika mchezo huo. Wiki iliyopita Aubameyang alikuwa ameweka rekodi ya kushinda katika mechi za mwanzo za Bundesliga na jana aliongeza rekodi hiyo kufikia mechi saba. Sare hiyo imeifanya Dortmund kuwa nyuma ya vinara wa Bundesliga Bayern Munich kwa alama nne, ambapo wanatarajiwa kucheza nao Jumapili ijayo.

No comments:

Post a Comment