Monday, September 28, 2015

GERRARD AIBEBA GALAXY.

NAHODHA wa zamani wa kimataifa wa Uingereza na klabu ya Liverpool, Steven Gerrard jana amefunga bao katika ushindi wa mabao 3-2 iliyopata klabu yake ya Los Angeles Galaxy dhidi ya FC Dallas ambao umewafanya kukwea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya Soka ya Marekani kanda ya Magharibi. Gerrard alifunga bao la tatu na kuifanya timu yake kuongoza kwa mabao 3-1 baada ya Giovani dos Santos na Robbie Keane kufunga mengine. Hilo linakuwa bao la pili kwa Gerrard katika mechi 10 ambazo ameichezea Galaxy mpaka sasa baada ya kufunga lingine katika mchezo wake wa kwanza Julai mwaka huu. Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 35 amesema hakuwa na tatizo lolote katika kujiamini kwake na anadhani goli alilofunga lilikuwa na umuhimu wake katika timu.

No comments:

Post a Comment