Monday, September 28, 2015

GARI LA RAIS WA PSG LASHAMBULIWA.

TAARIFA kutoka nchini Ufaransa zimedai kuwa gari la rais wa klabu ya Paris Saint-Germain-PSG, Nasser Al-Khelaifi limeshambuliwa kwa mawe wakati akiondoka katika Uwanja wa Beaujoire unaomilikiwa na Nantes, Jumamosi iliyopita. Mabingwa hao wa Ligue 1 waliendelea kujiimarisha kileleni kufuatia ushindi mnono wa mabao 4-1 katika mchezo huo lakini baadhi ya mashabiki wapatao 20 hawakufurahishwa na matokeo ya timu yao kufungwa hatua iliyopelekea kulishambulia gari la rais huyo. Klabu ya Nantes imeomba radhi kwa rais huyo wa PSG na kulaani vikali tukio hilo lililofanywa na watu wasiojulikana. Polisi wa mji huo walithibitisha kutokea kwa tukio hilo lakini hakuna taarifa zozote rasmi zilizopelekwa polisi na PSG walikataa kutoa kauli yeyote kuhusiana na hilo.

No comments:

Post a Comment