Monday, September 28, 2015

USM ALGER YAICHAPA AL HILAL.

KLABU ya USM Alger ya Algeria jana wamefanikiwa kupata ushindi muhimu katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa nusu fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al Hilal ya Sudan. Katika mchezo huo USM Alger ambao walikuwa wageni walitoka nyuma na kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Al Hilal ambao unawaweka katika nafasi nzuri ya kutinga fainali. Timu hizo zinatarajiwa kukutana tena Jumamosi ijayo katika mchezo wa marudiano ambapo kama USM wakifanikiwa kupata walau sare inaweza kuwavusha moja kwa moja katika hatua hiyo. Timu nyingine ya Sudan katika michuano hiyo Al Merreikh wao walifanikiwa kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya TP Mazembe ya DR Congo juzi ambapo nao wanatarajiwa kurudiana Jumapili ijayo huko Lubumbashi. Bingwa wa michuano hiyo anatarajiwa kupata kitita cha dola milioni 1.5 na nafasi ya kucheza michuano ya Kombe la Klabu Bingwa ya Dunia huko Japan.

No comments:

Post a Comment