Monday, September 28, 2015

SPURS YAMTIMUA MKURUGENZI WAKE WA UFUNDI.

KLABU ya Tottenham Hotspurs imetangaza kuachana na mkurugenzi wake wa ufundi Franco Baldini kwa maelewano. Baldini mwenye umri wa miaka 54 aliondoka AS Roma ya Italia kabla ya kuteuliwa kushika wadhifa huo na Spurs Juni mwaka 2013 akiwa kama msimamizi mkuu wa masuala ya usajili. Katika taarifa yake Spurs wamedai kuwa Baldini anaondoka kwenda kufanya shughuli nyingine nje ya soka na wanamtakia kila kheri. Baldini waliwahi kuwa meneja msaidizi wa Muitaliano mwenzake Fabio Capello wakati alipokuwa akiinoa timu ya taifa ya Uingereza.

No comments:

Post a Comment