Monday, September 28, 2015

NYOTA WA ASTON VILLA ACHAGUA KUITUMIKIA UINGEREZA.

KIUNGO wa klabu ya Aston Villa Jack Grealish amechagua kulitumikia taifa la Uingereza katika mechi za kimataifa badala ya Jamhuri ya Ireland. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 20 ameshaichezea timu ya taifa ya vijana ya umri wa miaka chini ya 21 ya Jamhuri ya Ireland lakini alikataa mwito wa kuitwa katika kikosi cha wakubwa ambacho kilikuwa na mchezo wa kirafiki dhidi Uingereza Juni mwaka huu. Grealish alianza kucheza soka la kulipwa rasmi akiwa kwa mkopo katika klabu ya Nottingham County wakati walipocheza na MK Dons Septemba mwaka 2013. Mara ya kwanza kuitumikia Villa ilikuwa ni Mei mwaka 2014 akitokea benchi katika mchezo dhidi ya Manchester City.

No comments:

Post a Comment