Monday, September 28, 2015

SILVA, KOMPANY, HART FITI KUIVAA BORUSSIA MONCHS.

KLABU ya Manchester City ina uhakika wa wachezaji majeruhi kurejea kuelekea katika mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Borussia Monchengladbach kesho kutwa. Nyota hao ambao wanatumainiwa kurejea tena uwanjani ni pamoja na David Silva, Vicent Kompany na golikipa Joe Hart. City walipoteza mchezo wao wa kwanza dhidi ya Juventus wiki mbili zilizopita na sasa wanahitaji alama tatu katika mchezo wao ujao ili waweze kuweka hai matumaini yao ya kusonga mbele katika kundi D ambalo linaongozwa na Sevilla na Juventus. Silva alikosa mechi tatu za mwisho za City kutokana na majeruhi ya nyonga lakini sasa anatarajiwa kuwepo katika mchezo wa Jumatano baada ya kuanza mazoezi vyema. Pia kuna habari nzuri kwa Hart na Kompany ambao wote walikuwa benchi katika mchezo wa juzi ambao walipokea kipigo kizito kutoka kwa Tottenham Hotspurs.

No comments:

Post a Comment